Tuesday, July 5, 2011

HII NDIO SAFU KAMILI YA REDS MISS ILALA 2011

Warembo wafuatao kutoka katika katika vituo viwili vya Dar City Centre na Tabata wamefanikiwa kupitishwa na Kamati ya Miss Ilala kuingia kwenye kambi ya Miss Ilala inayo anza tarehe 4 Julai 2011. Warembo watakutana katika hotel ya Lamada Jumatatu saa nne kwa kwa ajili ya semina na kukamilisha taratibu zote za usaili ikiwa ni pamoja na kuingia mikataba na Dar Metropolitan promotions.


1. Jenifer Kakolaki,                                                          12. Alexia William

13. Patricia Kajubi


3. Salha Israel                                                                 14. Lilian Paul


4. Diana John                                                                  15. Judith Mlingwa


5. Nasra Salim                                                                16. Cresencia Haule


6. Godliver Mwashamba                                                 17. Williet Wilson


7. Faizal Ally                                                                  18. Priscilla Mchemwa


8. Augostina Mshanga                                                    19. Ritha Cuthbert


9. Lilian Bryceson                                                           20. Maria John


10. Lilian William                                                            21. Edna Mnada


11. Mariam Manyanya


Shindano la Redds Miss Ilala 2011 linategemewa kufanyika siku ya Vunja jungu katika ukumbi ulioko katikati ya jiji la Dar es salam.


Mpaka sasa hivi wadhamini waliojitokeza kudhamini Shindano hilo ni Redds Original inayozalishwa na kiwanda cha Tanzania Breweries Limited ambao ndio wadhamini wakuu, wengine ni Vodacom Tanzania, Tanzania Standard Newspapers, Fabak Fashion, TV Sibuka, Maisha Club, na 88.4 Clouds FM na Paris Pub ya Tabata.


Watakapokuwa kambini warembo watajifunza mambo mbali mbali yanayohusu mashindano ya urembo, mambo ya kijamii, kiuchumi, kisiasa na kibiashara. Pia watajifunza namna ya kujitunza kama wasichana na kufanya shughuli za kijamii. Warembo pia wanategemewa kufanya michezo mbali mbali, kuonyesha vipaji na kufanya ziara ya kitalii.


Jackson M. Kalikumtima

No comments:

Post a Comment