BURUDANI NA MICHEZO

                       MAANDALIZI TAMASHA LA ZIFF YAANZA KUSHIKA KASI!
Maandalizi ya tamasha la 14 la ZIFF mwaka 2011 yanazidi kushika kasi ambapo kwa mwaka huu Msanii wa Muziki Kutoka nchini marekani Oriville Richard maarufu kama SHAGGY anatarajia kutumbuiza kwenye tamasha hilo litakaofanyika huko kisiwani Zanzibar kwenye ukumbi wa Ngome Kongwe.

KIUNGO MCHEZAJI WA BARCELONA SERGIO BUSQUEST AFUTIWA TUHUMA ZA KUMTUSI MARCELO!



Kwa Mujibu wa Mkurugenzi wa ZIFF Dr. DEAN NYALUSI tamasha hilo pamoja na kunogeshwa na waandaji wa Burudani nchini Tanzania Prime Time Promotion Pia zitaonyeshwa Filamu 71 kutoka nchi 39 na zitakazoonyeshwa kwa siku 10 za tamasha hilo.
Kiungo mchezaji wa klabu ya Barcelona Sergio Busquest amefutiwa tuhuma za kumtusi beki wa klabu ya Real Madrid Marcelo na kamati ya rufaa ya Shirikisho la Soka Barani Ulaya UEFA.

SPORTING CLUB BRAGA YA URENO USO KWA USO NA FC PORTO LIGI YA UROPA!


Kwa Mujibu wa taarifa ya UEFA iliyotolewa hapo jana Busquest amefutiwa tuhuma hizo na sasa atakuwa huru kucheza mchezo wa fainal ya klabu bingwa barani humo dhidi ya Manchester United hapo tarehe 28 ya mwezi huu.


Busquest alituhumiwa na klabu ya Madrid kwa kumwita Marcelo MOMO kwa lugha ya Kiispaniola lenye maana ya Nyani wakati Madrid ikicheza na Barcelona kwenye nusu fainal ya klabu bingwa barani humo.

Usiku huu Huko Jijini Dublin nchini Ireland kutapigwa mchezo wa fainal ya michuano ya ligi ya Uropa kwenye uwanja wa Aviva.
Mchezo Huo Ambao utazikutanisha Sporting Club Braga ya Ureno na Fc Porto unatarajia kuwa na upinzani Mkubwa huku kivutio kikubwa hii leo anatarajia kuwa Kocha wa Fc Porto Andre Villa Boas ambaye kama ataipa Porto Kombe hilo atakuwa kocha w kwanza kijana kuchukua ubingwa Uropa League barani Ulaya.