Sunday, January 22, 2012

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL ATEMBELEA MRADI WA MAJI WA CHIUMBATI NACHINGWEA, APOKEA KADI YA MWENYEKITI WA CHADEMA (W) NACHINGWEA!

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifurahia ngoma ya asili wakati akiwasili kwenye eneo la mradi wa maji wa Chiumbati Miembeni, wakati alipotembelea mradi huo wa Nachingwea Masasi, akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Lindi, jana Januari 20, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Meneja wa Mradi wa maji wa Chiumbati, Francis Fumbuka, wakati alipotembelea mradi huo unaoendelea na ujenzi Nachingwe akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Lindi, iliyoanza jana Januari 20, 2012. Kushoto ni mkewe, Mama Zakhia Bilal.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea kadi ya uanachama kutoka kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA wa Wilaya ya Nachingwea, Hassan Mkope, aliyejiengua katika chama hicho na kujiunga na CCM, wakati Makamu alipotembelea mradi wa maji wa Chiumbati Nachingwea, akiwa katika zaiara yake ya mkoa wa Lindi, jana januari 20, 2012.
Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akionyesha kadi ya CHADEMA baada ya kukabidhiwa na Hassan Mkope (kulia) aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA wa Wilaya ya Nachingwea, aliyeamua kujiengua na kujiunga na CCM. Makamu ameanza ziara yake katika Mkoa wa Lindi jana januari 20.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Lindi, Profesa Mtopea, akizungumza kutoa shukrani.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na wananchi wa Nachingwea, wakati alipokuwa akiondoka katika mradi wa maji wa Chiumbati jana, januari 20, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na wananchi wa Nachingwea, wakati alipokuwa akiondoka katika mradi wa maji wa Chiumbati jana, januari 20, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR.

No comments:

Post a Comment