Tuesday, August 2, 2011

TAARIFA YA TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA YAZINDULIWA!

Jitihada zinahitajika katika kuhakikisha watoto wanapata malezi bora ili kujinusuru kujiingiza katika matukio ya uhalifu ambayo yanakinzana na sheria za nchi kufuatia Takwimu kuonyesha wazazi na walezi ndio chanzo kikubwa kinachochangia watoto kujiingiza katika matukio ya maovu.

Akizungumza katika Uzinduzi wa Taarifa ya Tume ya haki za binadamu na utawala, Mkurugenzi wa Utafiti na Nyaraka, EPIPHANIA MFUNDO amesema hatua ya mtoto kuhukumiwa kifungo iwe ya mwisho ili kuondokana na ukatili kwa watoto magerezani.


Aidha Mkuu wa kitengo cha Jinsia na watoto kutoka Jeshi la polisi, Bi ZUHURA MUNISI amesema usasa, uweledi na polisi jamii ndio itakayoweza kuwajenga watoto katika maeneo yao kwa kushirikiana na jamii.

No comments:

Post a Comment