Tuesday, August 2, 2011

NIMEKUBALI HARUNA MOSHI HANA NIDHAMU - KOCHA WA STARS

KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya Taifa ‘Taifa Stars’ Jan Poulsen(pichani mwenye kofia) amekerwa na tabia ya utovu wa nidhamu iliyooneshwa na mchezaji Haruna Moshi ‘Boban’ ya kushindwa kuripoti katika kambi ya timu ya vijana ya chini ya miaka 23 iliyokuwemo jijini Arusha.

Poulsen aliwaita wachezaji watatu Gaudence Mwaikimba, Juma Seif ‘Kijiko’ na Boban kuja jijini Arusha kucheza michezo miwili ya kirafiki kati ya Vijana Stars na Shelisheli ili aangalie uwezo wao kama anaweza kuwaita katika kikosi cha Taifa Stars.


Akizungumza na waandishi wa habari mjini Arusha jana, Poulsen alisema ni mchezaji mmoja tu aliyeitikia mwito huo ambaye ni Kijiko, huku Mwaikimba akitoa taarifa kuwa ni mgonjwa lakini Boban hakukuwa na taarifa zozote juu yake.

Kocha huyo raia wa Denmark alisema, wakati wanaondoka Dar es Salaam mchezaji huyo alisema atakuja na usafiri wake binafsi lakini hadi sasa haijulikani alipo.


“Sijawahi kumwona Boban akicheza lakini niliambiwa ni mzuri na pia niliambiwa kuwa ni mchezaji ambaye hana nidhamu na kweli nimeliona hilo mwenyewe,”alisema.

No comments:

Post a Comment