Tuesday, August 2, 2011

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA KILIMO CHA ZABIBU DODOMA!

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, na mkewe Mama Asha Bilal, wakifurahia ngoma ya asili kabira la Wagogo, wakati walipowasili Kijiji cha Chilangali (ii) Wilaya ya Chamwino Mkoa wa Dodoma leo Agosti 02, 2011 kukagua mradi wa kilimo cha Zabibu (FUNE) katika shamba hilo lenye ukubwa wa Hekari 300.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na mkewe, wakiangalia Pikipiki aina ya Bajaj, aliyoizindua na kumkabidhi Mwenyekiti wa SACCOS ya FUNE, Jones Mazengo. Bajaj hiyo imetolewa na Benki ya CRDB ili itumike katika shughuli za kutembelea shamba la Mizabibu lililopo kijijini Chilangali (ii), likiwa na hekari 300 ambazo zinamilikiwa na wananchi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi funguo ya Bajaj, Mwenyekiti wa SACCOS ya FUNE, Jones Mazengo baada ya kuzindua rasmi leo Agosti 02, Bajaji hiyo iliyotolewa msaada na Benki ya CRDB kwa ajili ya kutumika kwa shughuli za kutembelea shamba la Mizzabibu lililopo kijiji cha Chilangali (ii) Wilaya ya Chamwino mkoa wa Dodoma, likiwa na ukubwa wa hekari 300.Katikati ni Mama Asha Bilal.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na mkewe, Mama Asha Bilal, wakiangalia Bwawa la kuhifadhia maji ya kumwagilia mashamba ya Zabibu, wakati walipowasili Kijiji cha Chilangali (ii) Wilaya ya Chamwino Mkoa wa Dodoma leo Agosti 02, 2011 kukagua mradi wa kilimo cha Zabibu (FUNE) katika shamba hilo lenye ukubwa wa Hekari 300. Picha na Muhidin Sufiani-OMR.

No comments:

Post a Comment