Tuesday, August 2, 2011

VOLCANO ZA VILELE VYA SHIRA NA MAWENZI MLIMA KILIMANJARO ZIMEKUFA!

Imebainika kwamba kadri miaka inavyokwenda ndivyo asili ya Mlima Kilimanjaro wenye vilele vitabu inapotea baada ya kuelezwa kuwa Volcano za vilele vya Shira na Mawenzi kufa na haziwezi kulipuka tena.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) DK TEREZYA LUOGA HUVISA amesema, tafiti mbalimbali za hivi karibuni zimebainisha volcano za vilele hivyo kufa na ile ya kilele cha Kibo imelala na kuna dalili bado ni hai.


Katika hatua nyingine Waziri HUVISA amesema kutokana na matukio ya milipuko ya hivi karibuni Wizara yake kwa kushirikiana na Shirika la Hifadhi za Taifa TANAPA inakusudia kutafuta wataalam wa milipuko ili kungalia uwezekano wa kulipuka tena.

No comments:

Post a Comment