Tuesday, August 2, 2011

MREMA AMSHUKIA CHIKU ABWAO KWA KUMWITA YEYE NI KIBARAKA WA CCM!

Mbunge wa Vunjo kupitia TLP Mheshimiwa AUGUSTINO LYATONGA MREMA amewaomba wabunge kujadili kero mbalimbali zinazowakabili wananchi wao badala ya kuzungumzia masuala binafsi yasiyo na tija kwa taifa.

Akijibu tuhuma zilizotolewa na Mbunge wa Viti Maalum (Chadema) CHIKU ABWAO bungeni kwamba yeye ni kibaraka wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mheshimiwa MREMA amesema hiyo ni kashfa na kwamba chama hicho hakihitaji msaada wowote kutoka kwake.


Katika hatua nyingine Mheshimiwa Mrema amebainisha kwamba ingawa baadhi ya wapinzani wanapinga uhuru wake wa kutoa maoni yeye haoni sababu ya kufanya hivyo kwani serikali iliyoko madarakani inatekeleza ahadi zake kama ilivyoahidi kwa wananchi wa Vunjo.

No comments:

Post a Comment