Tuesday, August 2, 2011

IDDI AZZAN AZUNGUMZIA MSONGAMANO WA MAGARI JIJINI DSM!

Licha ya juhudi inazofanya katika kutengeneza barabara nchini, Serikali imeombwa kushughulikia suala la msongamano wa magari Jijini Dar es Salaam kwa upendeleo mkubwa ili jiji hilo liendelee kutoa mchango katika kukuza uchumi wa Tanzania.

Mbunge wa Kinondoni Mheshimiwa IDD AZZAN amesema kwa kuwa Dar es Salaam imekuwa ikitoa karibia asilimia 80 ya pato la Taifa kuna kila sababu ya kuliongezea bajeti ya barabara ili liweze kukabiliana na msongamano wa magari unaoathiri ukuaji wa uchumi wake.


Kuhusiana fedha zitakazotumika kujenga barabara ya juu katika makutano ya barabara za Nyerere na Mandela Mheshimiwa AZZAN ametoa wito kwa serikali kutenga fedha za ndani badala ya kutegemea fedha kutoka kwa wahisani.

No comments:

Post a Comment