Tuesday, July 17, 2012

UNAJUA KWAMBA MILLARD AYO ALIWAHI KUTOLEWA KATIKA CHUMBA CHA MTIHANI KWA KUTOMALIZIA ADA?

Kama tulivyokuahidi msomaji wa Mo blog ifuatayo ni sehemu ya pili ya mahojiano kati ya Mhariri wa Mo Blog Lemmy Hipolite na Mtangazaji maarufu Millard Ayo.



Mo Blog: Tunamsikia Millard Ayo lakini hatujui ni nani hasa.?

Millard Ayo: Milliard Ayo ni kijana wa miaka 26 aliyezaliwa tarehe 26 Januari mwaka 1986 ni kijana aliyezaliwa katika hospitali ya Mount Meru na ni mtoto wa kwanza kwenye familia ya watoto wanne.

Ninatoka katika familia ya Mzee Arael Ayo al maarufu kama ‘Chalii’ pale Tengeru mkoani Arusha.

Mo Blog: Tupe siri ya mafanikio yako pamoja na umaarufu ulionao.?


Millard Ayo: Kiukweli moja kati ya vitu vinavyonifanya mimi nipate mafanikio, namshukuru Mungu kwa sababu kwanza situmii vitu vinavyowaangusha watu wengi kwenye kazi kama hizi; kwanza kabisa mimi sinywi pombe na sijawahi kunywa tangu nizaliwe; nadhani inanisaidia pia kwa sababu wakati wote akili inakuwa ‘fresh’.

Mo Blog: Kwa kifupi tuambie ilikuaje mara ya mwisho tumekusikia Radio One ghafla Clouds FM.?


Millard Ayo: Clouds Fm walivutiwa na kazi yangu, nadhani waliona uwezo wangu kupitia show ya ‘Milazo 101’ niliokuwa nikiifanya Radio One so alinipigia simu bosi wao nakumbuka ilikuwa ni siku ya Jumatano akaniambia tuonane.


Ukizingatia mimi nilikuwa na dream sana kufanya kazi ‘Clouds’ hata wakati naingia college ya Journalism nilikuwa na ndoto za kufanya kazi Clouds.


Kuendelea kusoma mahojiano haya zaidi ingia humu, www.mohammeddewji.com/blog

No comments:

Post a Comment