Sunday, October 9, 2011

WACHINA WALIVYOLETA TAFRANI MBEYA BAADA YA KULIPISHWA USHURU WA MAEGESHO WEEK END!

Moja ya watumishi wa kampuni ya AAICO ambayo ndiyo wamepewa dhamana ya kukusanya ushuru wa maegesho ya magari jijini Mbeya akitoa mnyororo kulifunga gari ya wachina hao huku mama wa kichina akilia kwa hasira.

Mama wa kichina akimtolea maneno makali binti Eliza mkusanya ushuru wa maegesho ya magari huku mchina huyo akiendelea kugoma kuwa hawezi lipa ushuru siku ya Jumamosi na Jumapili kwani ni siku za mapumziko siyo siku za kukusanya ushuru.
Mume wa mama mama wa kichina akijaribu nae kuwaelewesha wakusanyaji waushuru wa maegesho yamagari kuwa wameshazoea hivyo kutolipa siku ya Jumamosi na Jumapili kwani ni siku za mapumziko.
Mama wa Kichina kiwa amechachamaa na kuelekea katika Jengo la NMB Tawi la Mbalizi Road Mjini Mbeya kuomba msaada kwa mapolisi. Picha zaidi ya tukio hili tembelea: http://www.mbeyayetu.blogspot.com/.

No comments:

Post a Comment