Monday, June 6, 2011

MASHINDANO YA MBIO ZA KUOGELEA MITA 100 YALIVYOKUWA DSM!

Mkuu wa Udhamini wa Vodacom Tanzania George Rwehumbiza akimvalisha medali mshindi wa kuogelea mita 100 katika mashindano ya klabu bingwa Tanzania kwa washiriki chipukizi Agnes Kimimba.
Waogeleaji wa  timu ya KMKM kutoka Zanzibar kutoka kushoto Ally Hamiss,Omary Abdallah na Othman Ally wakibusu medali zao za dhahabu mara baada ya kutangazwa washindi wa klabu bingwa Tanzania kwa upande wa watu wazima,mashindano hayo  yamefanyika  Funkys masaki jijini Dares salaam na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania.
Katibu Mkuu wa TSA Noel Kiunsi akiwaangalia waogeleaji Ankitu Bhatt(15)na Macayla Buchanan(15)wa timu ya Stingray klabu ya jijini Dares Salaam wakishangilia ushindi wao  mara baada ya kutangazwa washindi wa kuogelea katika mashindano ya klabu bingwa Tanzania kwa waogeleaji chipukizi,mashindano hayo yalifanyika Funkys jijini Dares salaam na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania.
Katibu Mkuu wa TSA Noel Kiunsi(kushoto)na Ofisa mkuu mwendeshaji wa Vodacom Tanzania Peter Correia wakiwakabidhi kombe timu ya KMKM kutoka Zanzibar waliochukua ushindi wa mashindano ya klabu bingwa Tanzania kwa upande wa watu wazima,Mashindano hayo yalifanyika Funkys jijini Dares salaam na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania. Ofisa Mkuu mwendeshaji wa Vodacom Tanzania Peter Correia akiwakabidhi kombe wachezaji wa timu ya kuogelea ya KMKM kutoka Zanzibar kushoto Hanna Ally na Othman Abdallah baada ya kuwa washindi wa jumla wa mashindano ya klabu bingwa Tanzania,Mashindano hayo yalifanyika Funkys jijini Dares salaam na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania.

No comments:

Post a Comment