Monday, June 6, 2011

HAYA YALIKUPITA WEEK END HII JIJINI DAR ES SALAAM....TUNAKUKUMBUSHA!

Vodacom Miss Kurasini Mwajabu Juma akipunga mkono mara baada ya kutangazwa mshindi, kushoto mshindi wa pili Naifat Ally na mshindi wa tatu kulia Prisca Steven.

Afisa Udhamini wa Vodacom Tanzania Ibrahim Kaude akimkabidhi mshindi wa Vodacom Miss Kurasini Mwajabu Juma kiasi cha fedha taslimu cha shilingi 500,000, shindano hilo lilifanyika Jijini Dares Salaam.
Afisa Udhamini wa Vodacom Tanzania Ibrahim Kaude, akaiwaaga wachezaji wa timu ya Holy Family ya mkoa wa Ruvuma waliokuwa wakielekea Zanzibar kwenye mashindano ya Muungano Cup watapambana na mshindi wa Zanzibar kesho, kushoto Mratibu wa shindano hilo Daud Yassin. 
Mmoja wa wacheza wa timu ya Holy Family ya Mkoa wa Ruvuma akijaribu kumili mpira mbele ya Afisa udhamini wa Vodacom Tanzania Ibrahim Kaude na Mratibu wa shindano la Muungano mara baada ya kukabidhiwa mipira kwa ajili ya mchezo wa kesho na timu ya Zanzibar.

Baadhi ya washiriki wa mashindano ya kuogelea ya klabu bingwa Tanzania 2011 wakichumpa kwa kuanza mashindano hayo ya kilometa 200, yanayofanyika Funky Obitz Masaki na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania.

Mmoja wa washiriki wa shindano la kuogelea la klabu bingwa Tanzania 2011 akijitahidi kumaliza kilometa 200 katika shindano hilo linalofanyika Funky Obitz Masaki na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania.

Warembo tano bora waliofanyikiwa kuingia katika shindano la kumtafuta Vodacom Miss Kurasini ambapo Mwajabu Juma (9) ndiye alienyakua taji hilo.

No comments:

Post a Comment