Monday, June 6, 2011

JUMUIYA YA KIKRISTO TANZANIA (CCT) YATAKA SERIKALI ISIJIHUSISHE NA MAHAKAMA YA KADHI!

Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) imeitaka Serikali isijihusishe na suala la uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi hapa nchini isipokuwa suala hilo waachiwe waislamu wenyewe.

Hayo yamebainishwa Jijini DSM na mwenyekiti wa jumuiya hiyo Askofu Peter Kitula wakati alipokuwa akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusiana na maazimio yaliyofikiwa na Mkutano wa 45 wa Halmshauri kuu ya CCT.
Askofu huyo amesema Serikali inapaswa kujitoa katika suala hilo kwa sababu yenyewe haina dini, ingawa uanzishwaji wa mahakama hiyo ni jambo zuri linalowahusu waislamu hivyo linapaswa litenganishwe na shughuli za Mamlaka ya Uendeshaji wa nchi.

No comments:

Post a Comment