Tuesday, July 3, 2012

WANAFUNZI NA WALIMU WA SHULE YA MSINGI LUGALO WATEMBELEA BUNGE MJINI DODOMA LEO


Baadhi ya wanafunzi wa Darasa la saba wa Shule ya Msingi Lugalo ya Jijini Dar es Salaam, wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya walimu wao, nje ya Ukumbi wa Bunge Mjini Dodoma leo, wakati walipofika kutembelea na kujifunza shughuli za Bunge, wakiwa katika ziara yao ya Kimasomo. Wanafunzi hao wanatarajia kuondoka mjini Dodoma kesho Julai 4, kurejea jijini Dar es Salaam, baada ya kumaliza ziara yao hiyo, ikiwa ni pamoja na kutembelea Chuo Kikuu cha Dodoma. Picha zote na www.sufianimafoto.blogspot.com
Baadhi ya wanafunzi wa Darasa la saba wa Shule ya Msingi Lugalo ya Jijini Dar es Salaam, wakiwa kwenye Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma, leo wakati walipofika Bungeni hapo kwa ajili ya kutembelea na kujifunza shughuli za Bunge wakiwa katika ziara yao ya Mkoa wa Dodoma inayomalizika leo jioni.
Baadhi ya walimu wakipozi kwa picha na baadhi ya wanafunzi, nje ya Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma leo.
'Wabuge watarajiwa wa miaka ijayo', Baadhi ya wanafunzi wakipozi kwa picha nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma leo.
Miongoni mwa wanafunzi hawa, wapo Walimu, Mawaziri, Makatibu, Madaktari, Wabunge na Viongozi mbalimbali wa miaka ijayo, endapo watapewa misingi ya elimu iliyo bora na kupewa elimu ya Nidhamu na utiifu wakiwa bado wadogo, ili waje kuwa viongozi bora siku za baadaye.

No comments:

Post a Comment