Sunday, January 8, 2012

KCB TANZANIA YAISAIDIA WODI YA ICU HOSPITAL KCMC!

Meneja wa KCB Tanzania Tawi la Moshi Bw Lomnyaki Saitabau akizungumza wakati akikabidhi wodi ya wagonjwa mahututi ‘ICU’ ya Hospitali ya KCMC iliyokarabatiwa na benki hiyo kwa gharama ya shilingi milioni 11/-. Anayeaangalia ni Daktari Bingwa wa magonjwa ya kinamama wa Hospitali hiyo Dk Gerald Masenga.
Meneja wa KCB Tanzania Tawi la Moshi Bw Lomnyaki Saitabau akizungumza wakati akikabidhi wodi ya wagonjwa mahututi ‘ICU’ ya Hospitali ya KCMC iliyokarabatiwa na benki hiyo kwa gharama ya shilingi milioni 11/-. Kulia ni Daktari Bingwa wa magonjwa ya kinamama wa Hospitali hiyo Dk Gerald Masenga.
Daktari Bingwa wa magonjwa ya kinamama wa Hospitali ya KCMC Moshi Dk Gerald Masenga akifurahia jambo wakati Benki ya KCB Tanzania tawi la Moshi ilipokabidhi wodi ya wagonjwa mahututi ‘ICU’ baada ya kuikarabati kwa gharama ya shilingi milioni 11/-. Wengine ni baadhi ya wauguzi wa hospitali hiyo.
Muuguzi Mkuu wa wa Hospitali ya KCMC Moshi Redempta Mamseti akifafanua jambo wakati Benki ya KCB Tanzania ilipokabidhi wodi ya wagonjwa mahututi ‘ICU’ baada ya kuikarabati kwa gharama ya shilingi milioni 11/-. Kulia ni Meneja wa Benki hiyo tawi la Moshi Bw Lomnyaki Saitabau.
Meneja wa KCB Tanzania Tawi la Moshi Bw Lomnyaki Saitabau akikata utepe kuzindua rasmi wodi ya wagonjwa mahututi ‘ICU’ ya Hospitali ya KCMC waliyoikarabati kwa gharama ya shilingi milioni 11/-. Anayeshudia (Kulia) ni Daktari Bingwa wa magonjwa ya kinamama wa Hospitali hiyo Dk Gerald Masenga.

No comments:

Post a Comment