Tuesday, August 2, 2011

ZOMBE AMTUHUMU LEMA KUHUSIKA NA MTANDAO WA WIZI WA MAGARI!

Aliyewahi kuwa mkuu wa upelelezi wa mkoa wa DSM ABDALAH ZOMBE ameibua tuhuma dhidi ya mbunge wa ARUSHA mjini GODBLESS LEMA zikiwa zimepita siku chache baada mbunge huyo kuhoji bungeni namna kesi ilivyokuwa ikimkabili ZOMBE ilivyoendeshwa.

Bwana ZOMBE alizungumza na waandishi wa habari nje ya Mahakama Kuu ya Tanzania hapo jana. Aidha zombe amedai kuwa wakati alipokuwa mkuu wa upelelezi mkoa wa DSM alipata taarifa kuwa Bwana LEMA ana mtandao wa wizi wa magari kutoka Tanzania na kuyapeleka Kenya.


Hata hivyo Mbunge wa ARUSHA mjini Bwana GODBLES LEMA amekanusha kuhuisna na madai hayo ya wizi wa magari.

No comments:

Post a Comment