Saturday, August 13, 2011

WREMBO WA VODACOM MISS TANZANIA WAINGIA KATIKA JUMBA LA VODACOM!


Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba akiwakaribisha mshiriki shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, Mariaclara Mathayo katika Jumba la Vodacom ambalo litatumika katika kipindi chote cha warembo wakiwa kambini. Katikati ni Mkurugenzi wa Lino International Agency, Waandaaji wa Vodacom Miss Tanzania, Hashim Lundenga. Warembo hao wameingia katika Jumba hilo Dar es Salaam jana.
Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba akimkaribisha mshiriki wa shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, Cynthia Kimasha katika Jumba la Vodacom ambalo litatumika katika kipindi chote cha warembo wakiwa kambini. Katikati ni Mkurugenzi wa Lino International Agency, Waandaaji wa Vodacom Miss Tanzania, Hashim Lundenga. Warembo hao wameingia katika Jumba hilo rasmi Dar es Salaam jana.
Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba (katikati) akiwafundisha namna ya kufungua shampeni warembo wanaoshiriki shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, muda mfupi baada ya warembo hao 30 kuingia katika Jumba la Vodacom lililopo jijini Dar es Salaam jana.
Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba (katikati) akigonganisha chupa za shampeini na warembo wanaoshiriki shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, muda mfupi baada ya warembo hao 30 kuingia katika Jumba la Vodacom lililopo jijini Dar es Salaam jana.
Warembo wanaoshiriki shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, wakigonganisha glasi zao za shampeni muda mfupi baada ya warembo hao 30 kuingia katika Jumba la Vodacom lililopo jijini Dar es Salaam jana.
Warembo wanaoshiriki shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, wakicheza kwaito wakati wa tafrija maalum ya kuwakaribisha katika Jumba la Vodacom lililopo jijini Dar es Salaam jana. Jumla ya warembo 30 waliingia katika jumba hilo kwa kambi yao.
Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba akizungumza jambo na warembo wanaoshiriki shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, baada ya kuingia katika Jumba la Vodacom jijini Dar es Salaam jana. (Picha na Mpigapicha wetu).

No comments:

Post a Comment