Wednesday, July 6, 2011

SPIKA MAKINDA ATOLEA UFAFANUZI OFISI ZA BUNGE ZANZIBAR!

Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ANNE MAKINDA ametolea ufafanuzi wa madai ya Wabunge wa Baraza la Wawakilishi kuhusiana na Ofisi za Bunge Zanzibar kutotumika na wabunge hao kama ilivyo kwenye ofisi ndogo za jijini Dar es Salaam.

Akijibu hoja kabla ya kuahirisha kikao cha bunge kipindi cha maswali na majibu Spika MAKINDA amesema kwa sasa ofisi hizo hazikidhi haja hivyo serikali ipo katika mchakato wa kusimamia ujenzi wa Ofisi ndogo za Bunge nchi nzima ikiwemo kuweka maofisa wa kutosha.


RAJABU MBAROUK MOHAMMED Mbunge wa Ole kwa tiketi ya (CUF) akichangia hoja ya makadirio ya matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais alihoji ofisi za bunge Zanzibar kutotoa huduma kwa waheshimiwa wabunge kama ilivyoanishwa kwenye katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

No comments:

Post a Comment