Monday, July 18, 2011

CHADEMA YATAKA MADIWANI WAKE ARUSHA WAJIUZULU!

Chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA kimetoa tamko la kutaka madiwani wake mkoani Arusha kujiuzulu nyadhifa zao ambazo walizipata wakati wa maridhiano ya kumpata naibu meya wa Arusha, kufuatia uchaguzi wake kuwa na utata mkubwa hivi karibuni.

Kauli hiyo imetolewa jijini Dar es Salaam Katibu mkuu wa CHADEMA Dakta WILLBROAD SLAA wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na maazimio ambayo yamefikiwa na kamati kuu ya chama hicho iliyoketi hivi karibuni.


Katika hatua nyingine Chadema imekanusha kujadili na kutoa maamuzi kuhusu sakata la Mbunge wa Jimbo la Maswa Magharibi JOHN SHIBUDA la kutoafiki azimio la Chama hicho la kuwataka wabunge wake kuzikataa Posho zao katika vikao vya Bunge linaloendelea Mjini Dodoma.

No comments:

Post a Comment